24 Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi;uliwashinda wakazi wa nchi hiyo,Wakanaani, ukawatia mikononi mwao,pamoja na wafalme wao,watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.
25 Miji yenye ngome wakaiteka,wakachukua nchi yenye utajiri,majumba yenye vitu vingi vizuri,visima vilivyochimbwa,mashamba ya mizabibu na mizeitunipamoja na miti yenye matunda kwa wingi.Hivyo wakala,wakashiba na kunenepana kuufurahia wema wako.
26 Lakini hawakuwa waaminifu kwako.Wakakuasi,wakaiacha sheria yakona kuwaua manabii waliowaonyaili wakurudie wewe.Wakakufuru sana.
27 Hivyo, ukawatia katika mikono ya adui zao,nao wakawatesa.Lakini wakiwa katika mateso yao,wakakulilia, nawe ukawasikia kutoka mbinguni.Na kwa huruma zako nyingi,ukawapelekea viongozi wa kuwaokoa;nao wakawakomboa toka mikononi mwao.
28 Lakini amani ilipopatikanawakatenda dhambi tena mbele yako,nawe ukawaacha watiwe katikamikono ya adui zao wawatawale.Hata hivyo, walipotubu na kukuliliaukawasikiliza kutoka mbinguni.Na kwa kulingana na huruma zako nyingi,ukawaokoa mara nyingi.
29 Ukawaonya ili wairudie sheria yako.Hata hivyo, kwa kiburi chao,wakaacha kuzitii amri zako.Wakayaasi maagizo yako,ambayo kwayo mtu akiyatii, ataishi.Wakawa wajeuripia wakafanya shingo zao ngumu,na wakakataa kuwa watiifu.
30 Ukawavumilia kwa miaka mingi,na kuwaonya kwa njia ya roho yakokwa kupitia manabii wako;hata hivyo hawakusikiliza.Basi ukawaachaukawatia mikononi mwa mataifa mengine.