18 mumbi, mwari, mderi,
19 korongo, aina zote za koikoi, hudihudi na popo.
20 “Wadudu wote wenye mabawa na waendao kwa miguu minne, hao ni najisi kwenu.
21 Lakini, baadhi ya wadudu wenye mabawa na wanakwenda kwa miguu minne ya kurukia ardhini mnaweza kula.
22 Hao ni: Kila aina ya nzige, kila aina ya senene, kila aina ya panzi na kila aina ya parare.
23 Lakini wadudu wengine wote wenye mabawa na miguu minne ni najisi kwenu.
24 “Kugusa wanyama fulanifulani humfanya mtu kuwa najisi; yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.