7 Limeiharibu mizabibu yetu,na kuitafuna mitini yetu.Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini,na matawi yake yameachwa meupe.
8 Lieni kama msichana aliyevaa vazi la guniaakiombolezea kifo cha mchumba wake.
9 Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.
10 Mashamba yamebaki matupu;nchi inaomboleza,maana nafaka imeharibiwa,divai imetoweka,mafuta yamekosekana.
11 Ombolezeni enyi wakulima;pigeni yowe enyi watunza mizabibu.Ngano na shayiri zimeharibika,mavuno yote shambani yameangamia.
12 Mizabibu imenyauka;mitini imedhoofika;mikomamanga, mitende na mitofaa imekauka,naam miti yote shambani imekauka.Furaha imetoweka miongoni mwa watu.
13 Enyi makuhani, jivikeni magunia kuomboleza,lieni enyi wahudumu wa madhabahu.Ingieni hekaluni mkaomboleze usiku kucha!Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mungu.