Mt.
Sura 9:18-24
Swahili Union Version
18 Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, Binti yangu sasa hivi amekufa; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi.
19Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake.
20Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.
21Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.
22Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.
23Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo,
24akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.