1 BWANA akamwambia Musa, akisema,
2 Sema na Haruni, na wanawe, na wana wote wa Israeli, ukawaambie; Neno hili ndilo aliloliamuru BWANA, akisema,
3 Mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli atakayechinja ng’ombe, au mwana-kondoo, au mbuzi, ndani ya marago, au atakayemchinja nje ya marago,
4 wala hamleti mlangoni pa hema ya kukutania, ili amtoe kuwa matoleo kwa BWANA mbele ya hema ya BWANA; mtu huyo atahesabiwa kuwa ana hatia ya damu; amemwaga damu; na mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake;