5 Lakini kama hamtaki kusikia maneno haya, mimi naapa kwa nafsi yangu, asema BWANA, ya kuwa nyumba hii itakuwa ukiwa.
6 Kwa maana BWANA asema hivi, katika habari ya nyumba ya mfalme wa Yuda;Wewe u Gileadi kwangu,na kichwa cha Lebanoni;Ila hakika nitakufanya kuwa jangwa,na miji isiyokaliwa na watu.
7 Nami nitakufanyia tayari watu wenye kuharibu,kila mtu na silaha zake;Nao watakata mierezi miteule yako,na kuitupa motoni.
8 Na mataifa mengi watapita karibu na mji huu, nao watasema kila mtu na jirani yake, Nini maana yake BWANA kuutenda hivi mji huu mkubwa?
9 Ndipo watakapojibu, Ni kwa sababu waliliacha agano la BWANA, Mungu wao, wakaabudu miungu mingine, na kuitumikia.
10 Msimlilie aliyekufa, wala msimwombolezee,Bali mlilieni huyo aendaye zake mbali;Kwa maana yeye hatarudi tena,Wala hataiona nchi aliyozaliwa.
11 Maana BWANA asema hivi, katika habari za Shalumu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; aliyemiliki badala ya Yosia, baba yake, yeye aliyetoka mahali hapa; Hatarudi huku tena;