1 Habari za Moabu. BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ole wake Nebo! Kwa maana umeharibika; Kiriathaimu umeaibishwa, umetwaliwa; Misgabu umeaibishwa, nao umebomolewa.
2 Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njoni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Sauti ya kilio toka Horonaimu,Ya kutekwa na uharibifu mkuu.
4 Moabu umeharibika;Wadogo wake wamewasikiza watu kilio.
5 Kwa maana watu wapandapo huko LuhithiWatapanda wasiache kulia;Nao watu watelemkapo huko HoronaimuWameisikia huzuni ya kilio cha uharibifu.
6 Haya! Kimbieni! Jiokoeni nafsi zenu!Mkawe kama mtu aliye mkiwa.