33 Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.
34 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!
35 Mwambieni Mwenyezi-Mungu:Utuokoe, ee Mungu wa wokovu wetu,utukusanye pamoja na kutuokoa kutoka kwa mataifa,tupate kulisifu jina lako takatifu,kuona fahari juu ya sifa zako.
36 Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,tangu milele na hata milele!Kisha watu wote wakasema, “Amina!” Pia wakamsifu Mwenyezi-Mungu.
37 Hivyo, mfalme Daudi akawaacha Asafu na nduguze Walawi mahali walipoliweka sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya huduma zinazotakiwa mbele ya sanduku kila siku.
38 Obed-edomu, mwana wa Yeduthuni, pamoja na wenzake sitini na wanane waliwasaidia. Obed-edomu mwana wa Yeduthuni na Hosa walikuwa walinzi wa malango.
39 Mfalme Daudi akawaweka kuhani Sadoki na makuhani wenzake kuwa wahudumu wa hema ya Mwenyezi-Mungu iliyokuwa mahali pa kuabudu huko Gibeoni