11 Utalipaka sanduku hilo dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu pande zote.
12 Kisha utalitengenezea pete nne na kuzitia miguuni pake, kila mguu pete moja.
13 Utatengeneza mipiko ya mjohoro na kuipaka dhahabu.
14 Mipiko hiyo utaipitisha katika pete zilizo pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibebea.
15 Mipiko hiyo itabaki daima katika pete; isitolewe wakati wowote.
16 Ndani ya sanduku hilo utaweka vibao viwili vya mawe vya ushuhuda.
17 “Kisha utatengeneza kwa dhahabu safi kiti cha rehema, urefu wake sentimita 110, na upana wake sentimita 66.