20 Viumbe hivyo vitaelekeana, mabawa yake yamekunjuka kukifunika kiti cha rehema; nyuso zake zitaelekea kiti hicho.
21 Ndani ya sanduku utaweka vibao viwili vya mawe na kukiweka kiti cha rehema juu yake.
22 Mimi nitakutana nawe hapo; na kutoka juu ya kiti hicho cha rehema katikati ya viumbe hao walioko juu ya sanduku la ushuhuda, nitazungumza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.
23 “Utatengeneza meza ya mbao za mjohoro yenye urefu wa sentimita 88, upana sentimita 44 na kimo sentimita 66.
24 Hiyo meza utaipaka dhahabu safi na kuizungushia utepe wa dhahabu.
25 Kisha utaizungushia ubao wenye upana wa sentimita 66.
26 Utaitengenezea pete nne za dhahabu na kuzitia kwenye pembe zake miguuni pake.