24 Anayeiba mali ya baba yake au mama yake, akasema si kosa,hana tofauti yoyote na wezi wengine.
25 Mchoyo huchochea ugomvi,lakini anayemtegemea Mwenyezi-Mungu atafanikiwa.
26 Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mpumbavu;lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.
27 Aliye mkarimu kwa maskini hatatindikiwa kitu,lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.
28 Waovu wakitawala watu hujificha,lakini wakiangamia, waadilifu huongezeka.