1 Siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda;Sisi tunao mji ulio na nguvu;Ataamuru wokovu kuwa kuta na maboma.
2 Wekeni wazi malango yake,Taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie.
3 Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemeaKatika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.
4 Mtumainini BWANA siku zoteMaana BWANA YEHOVA ni mwamba wa milele.
5 Kwa kuwa amewashusha wakaao juu,Mji ule ulioinuka, aushusha,Aushusha hata nchi, auleta hata mavumbini.
6 Mguu utaukanyaga chini,Naam, miguu yao walio maskini,Na hatua zao walio wahitaji.