25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, walimpeleka mtoto kwa kuhani Eli.
26 Hana akamwambia, “Ee bwana wangu, kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mimi ndimi yule mwanamke aliyekuwa anasimama mbele yako akimwomba Mwenyezi-Mungu.
27 Nilimwomba anipe mtoto huyu, na yeye alinipa kile nilichomwomba.
28 Kwa sababu hiyo, mimi ninampa Mwenyezi-Mungu mtoto huyu; wakati wote atakapokuwa hai, ametolewa kwa Mwenyezi-Mungu.” Halafu, wakamwabudu Mwenyezi-Mungu hapo.