1 Halafu Hana aliomba na kusema:“Namshangilia Mwenyezi-Mungu moyoni mwangu.Namtukuza Mwenyezi-Mungu aliye nguvu yangu.Nawacheka adui zangu;maana naufurahia ushindi wangu.
2 “Hakuna aliye mtakatifu kama Mwenyezi-Mungu;hakuna yeyote aliye kama yeye;hakuna aliye mwamba kama Mungu wetu.
3 Acheni kujisifu,acheni kusema ufidhuli.Maana ajuaye ni Mwenyezi-Mungu.Yeye huyapima matendo yote.
4 Pinde za wenye nguvu zimevunjika.Lakini wadhaifu wanaendelea kupata nguvu.