1 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,
2 “Waambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo, nawe upokee kwa niaba yangu. Utapokea kutoka kwa mtu yeyote atakayetoa kwa moyo mkunjufu.
3 Utapokea matoleo yafuatayo: Dhahabu, fedha, shaba,
4 sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa manyoya ya mbuzi;