3 Utapokea matoleo yafuatayo: Dhahabu, fedha, shaba,
4 sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa manyoya ya mbuzi;
5 ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi, mbao za mjohoro,
6 mafuta kwa ajili ya taa, viungo kwa ajili ya mafuta ya kuweka wakfu na kwa ajili ya ubani wenye harufu nzuri,
7 vito vya sardoniki, na vito vingine kwa ajili ya mapambo ya kizibao cha kuhani na kifuko cha kifuani.
8 Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, ili niweze kukaa kati yao.
9 Utatengeneza hema hiyo na vifaa vyake kulingana na mfano nitakaokuonesha.