15 “Utatengeneza mbao za mjohoro za kusimama wima kwa ajili ya hema.
16 Kila ubao utakuwa na urefu wa mita 4, na upana wa sentimita 66.
17 Kila ubao utakuwa na ndimi mbili za kuunganishia. Utazifanyia mbao zote ndimi mbili.
18 Basi, utatengeneza hizo mbao za hema hivi: Mbao ishirini kwa ajili ya upande wa kusini,
19 na vikalio arubaini vya fedha chini ya hizo mbao ishirini, vikalio viwili chini kwa kila ubao ili kushikilia zile ndimi zake mbili na vikalio viwili viwe chini ya ubao mwingine ili kushikilia zile ndimi zake mbili.
20 Upande wa kaskazini wa hema, utatengeneza mbao ishirini,
21 na vikalio vyake arubaini vya fedha, vikalio viwili chini ya kila ubao.