1 Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.
2 Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji.
3 Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa.
4 Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza,