Mdo
Sura 5:17-23
Swahili Union Version
17 Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,
18wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;
19lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,
20Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.
21Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha.Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.
22Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari,
23wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.