12 Umenijazi uhai na upendeleo,Na maangalizi yako yameilinda roho yangu.
13 Lakini mambo haya uliyaficha moyoni mwako;Najua kuwa haya yamo nafsini mwako;
14 Nikifanya dhambi, ndipo waniangalia,Wala hutaniachilia na uovu wangu.
15 Mimi nikiwa mbaya, ole wangu!Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu;Mimi nimejaa aibuNa kuyaangalia mateso yangu.
16 Kichwa changu kikijiinua, waniwinda kama simba;Tena wajionyesha kwangu kuwa wa ajabu.
17 Wewe warejeza upya hao mashahidi yako juu yangu,Na kasirani yako waiongeza juu yangu;Jeshi kwa jeshi juu yangu.
18 Kwa nini basi kunitoa tumboni?Ningekata roho, lisinione jicho lo lote.