Ayu.
Sura 10:15-21
Swahili Union Version
15 Mimi nikiwa mbaya, ole wangu!Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu;Mimi nimejaa aibuNa kuyaangalia mateso yangu.
16 Kichwa changu kikijiinua, waniwinda kama simba;Tena wajionyesha kwangu kuwa wa ajabu.
17Wewe warejeza upya hao mashahidi yako juu yangu,Na kasirani yako waiongeza juu yangu;Jeshi kwa jeshi juu yangu.
18Kwa nini basi kunitoa tumboni?Ningekata roho, lisinione jicho lo lote.
19Ningalikuwa kama mtu asiyekuwapo;Ningalichukuliwa kaburini kutoka tumboni.
20 Je! Siku zangu si chache? Acha basi,Usinisumbue, nipate ngaa kutuzwa moyo kidogo.
21 Kabla sijaenda huko ambako sitarudi kutoka huko tena,Ni hiyo nchi ya giza, giza tupu;