19 Ningalikuwa kama mtu asiyekuwapo;Ningalichukuliwa kaburini kutoka tumboni.
20 Je! Siku zangu si chache? Acha basi,Usinisumbue, nipate ngaa kutuzwa moyo kidogo.
21 Kabla sijaenda huko ambako sitarudi kutoka huko tena,Ni hiyo nchi ya giza, giza tupu;
22 Ni nchi ya giza kuu, kama giza lenyewe lilivyo;Ni nchi ya giza tupu, isiyo na matengezo ya mambo yo yote,Nchi ambayo nuru yake ni kama giza.