1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu, na kusema,
2 Je! Huu wingi wa maneno usijibiwe?Na mtu aliyejaa maneno, je! Ahesabiwe kuwa na haki?
3 Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya?Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?
4 Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi,Nami ni safi machoni pako.
5 Lakini, laiti Mungu angenena,Na kuifunua midomo yake juu yako;
6 Tena akuonyeshe hizo siri za hekima,Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake!Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.
7 Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?