16 Kwa kuwa utasahau mashaka yako;Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita;
17 Na maisha yako yatakuwa meupe kuliko adhuhuri;Lijapokuwa ni giza, litakuwa kama alfajiri.
18 Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini;Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama.
19 Tena utalala, wala hapana atakayekutia hofu;Naam, wengi watakutafuta uso wako.
20 Lakini macho ya waovu yataingia kiwi,Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia,Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho.