5 Laiti mngenyamaza kabisa!Hilo lingekuwa hekima kwenu.
6 Sikieni sasa basi hoja zangu,Mkayasikie mashindano ya midomo yangu.
7 Je! Mtanena yasiyo ya haki kwa ajili ya Mungu,Na kusema kwa udanganyifu kwa ajili yake?
8 Je! Mtamwonyesha yeye upendeleo?Mtamtetea Mungu?
9 Je! Itafaa yeye kuwatafuta ninyi?Au, kama kumdanganya mtu, je! Mtamdanganya yeye?
10 Hakika atawakemea ninyi,Mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Je! Huo ukuu wake hautawatia hofu,Na utisho wake hautawaangukia?