6 Acha kumwangalia yeye, apate kupumzika,Hata atakapoitimiza siku yake, kama aliyeajiriwa.
7 Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena,Wala machipukizi yake hayatakoma.
8 Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani,Na shina lake kufa katika udongo;
9 Lakini kwa harufu ya maji utachipuka,Na kutoa matawi kama mche.
10 Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia;Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?
11 Kama vile maji kupwa katika bahari,Na mto kupunguka na kukatika;
12 Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke;Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka,Wala kuamshwa usingizini.