1 Ndipo Elifazi, Mtemani, akajibu, na kusema,
2 Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio,Na kujaza tumbo lake na upepo wa mashariki?
3 Je! Ahoji na mazungumzo yasiyo faida,Au kwa maneno ambayo hawezi kufanya mema kwayo?
4 Naam, wewe waondoa kicho,Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.