10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu;Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.
11 Huwatoa kama kundi watoto wao.Na watoto wao hucheza.
12 Huimba kwa matari na kwa kinubi,Na kuifurahia sauti ya filimbi.
13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa,Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee;Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie?Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao;Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.