15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie?Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao;Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa?Na msiba wao kuwajilia?Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?
18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo,Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?
19 Mwasema, Mungu huwawekea watoto wa mtu huo uovu wake.Na amlipe mwenyewe, ili apate kuujua.
20 Macho yake mwenyewe na yaone uharibifu wake,Akanywe ghadhabu zake Mwenyezi.
21 Kwani ana furaha gani katika mbari yake baada yake,Hesabu ya miezi yake itakapokwisha katwa katikati?