2 Yasikizeni sana maneno yangu;Jambo hili na liwe faraja yenu.
3 Niacheni, nami pia nitanena;Tena nikiisha nena, zidini kudhihaki.
4 Mimi, je! Mashitaka yangu yamhusu mwanadamu?Nami kwa nini nisikose kusubiri?
5 Niangalieni, mkastaajabu,Mkaweke mkono kinywani.
6 Hata nikumbukapo nahuzunika,Na utisho wanishika mwilini mwangu.
7 Mbona waovu wanaishi,Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?
8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao,Na wazao wao mbele ya macho yao.