22 Je! Mtu awaye yote atamfundisha Mungu maarifa?Naye ndiye awahukumuye walioko juu.
23 Mmoja hufa katika nguvu zake kamili,Mwenye kukaa salama na kustarehe;
24 Vyombo vyake vimejaa maziwa,Na mafuta ya mifupani mwake ni laini.
25 Mwingine hufa katika uchungu wa roho,Asionje mema kamwe.
26 Wao hulala mavumbini sawasawa,Mabuu huwafunika.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu,Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.
28 Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi?Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?