4 Ningeiweka daawa yangu mbele yake,Na kukijaza kinywa changu hoja.
5 Ningeyajua maneno atakayonijibu,Na kuelewa na hayo atakayoniambia.
6 Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake?La, lakini angenisikiliza.
7 Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye;Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.
8 Tazama, naenda mbele, wala hayuko;Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona;
9 Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona;Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone.
10 Lakini yeye aijua njia niendeayo;Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.