1 Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi?Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?
2 Wako waziondoao alama za mipaka;Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
3 Humfukuza punda wake asiye baba,Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
4 Humgeuza mhitaji aiache njia;Maskini wa nchi hujificha pamoja.