1 Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,
2 Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya kale,Kama katika siku hizo Mungu aliponilinda;
3 Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani,Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;
4 Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa,Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu;