7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani?Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe;Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
9 Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia;Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.
10 Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu,Awapaye nyimbo wakati wa usiku;
11 Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi,Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani?
12 Hulia huko, lakini hapana ajibuye,Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
13 Hakika Mungu hatasikia ubatili,Wala Mwenyezi hatauangalia.