21 Jitunze, usiutazame uovu;Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu.
22 Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake;Ni nani afundishaye kama yeye?
23 Ni nani aliyemwagiza njia yake?Au ni nani awezaye kusema, Wewe umetenda yasiyo haki?
24 Kumbuka kuitukuza kazi yake,Watu waliyoiimbia.
25 Wanadamu wote wameitazama;Watu huiangalia kwa mbali
26 Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui;Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Kwani yeye huvuta juu matone ya maji,Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;