26 Kunyesha mvua juu ya nchi isiyo na watu;Juu ya jangwa asiyokaa mwanadamu;
27 Kuishibisha nchi iliyo kame na ukiwa,Na kuyameza majani yaliyo mororo?
28 Je! Mvua ina baba?Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande?
29 Barafu ilitoka katika tumbo la nani?Na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa?
30 Maji hugandamana kama jiwe,Na uso wa vilindi huganda kwa baridi.
31 Je! Waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia,Au kuvilegeza vifungo vya Orioni?
32 Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake?Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake?