9 Nilipolifanya wingu kuwa vazi lake,Na giza zito kuwa nguo ya kuifungia,
10 Nikaiagiza amri yangu;Nikaiwekea makomeo na milango,
11 Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita,Na hapa mawimbi yako yanyetayo yatazuiliwa?
12 Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza?Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?
13 Yapate kuishika miisho ya nchi,Waovu wakung’utwe wakawe mbali nayo?
14 Hubadilika mfano wa udongo chini ya muhuri,Vitu vyote vinatokea kama mavazi.
15 Na waovu nuru yao huzuiliwa isiwafikie,Na mkono ulioinuka huvunjika.