13 Wafiche mavumbini pamoja,Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.
14 Ndipo mimi nami nitazikiri habari zako,Ya kuwa mkono wako wa kuume waweza kukuokoa.
15 Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe;Yeye hula nyasi kama vile ng’ombe,
16 Tazama basi, nguvu zake ni katika viuno vyake,Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake.
17 Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi;Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.
18 Mifupa yake ni kama mirija ya shaba;Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.
19 Yeye ni mkuu wa njia za Mungu;Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake.