16 Basi hivi huyo maskini ana matumaini,Na uovu hufumba kinywa chake.
17 Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye;Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.
18 Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza;Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.
19 Yeye atakuokoa na mateso sita;Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.
20 Wakati wa njaa atakukomboa na mauti;Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
21 Utafichwa na mapigo ya ulimi;Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.
22 Wewe utayacheka maangamizo na njaa;Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.