3 Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi;Lakini mara niliyalaani maskani yake.
4 Watoto wake wako mbali na wokovu,Nao wamesongwa langoni,Wala hapana atakayewaponya.
5 Mavuno yake wale wenye njaa huyala,Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani,Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.
6 Kwani taabu haitoki mchangani,Wala mashaka hayachipuki katika nchi;
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka,Kama cheche za moto zirukavyo juu.
8 Lakini mimi ningemtafuta Mungu,Ningemwekea Mungu daawa yangu;
9 Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;