9 Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;
10 Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi,Na kuyapeleka maji mashambani;
11 Awainuaye juu hao walio chini;Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.
12 Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu,Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe;Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana,Hupapasa mchana vilevile kama usiku.
15 Lakini yeye huokoa na upanga wa kinywa chao,Hata kumwokoa mhitaji na mkono wake aliye hodari.