3 Kama akipenda kushindana naye,Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu;Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?
5 Aiondoaye milima, nayo haina habari,Akiipindua katika hasira zake.
6 Aitikisaye dunia itoke mahali pake,Na nguzo zake hutetema.
7 Aliamuruye jua, nalo halichomozi;Nazo nyota huzipiga muhuri.
8 Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu,Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
9 Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia,Na makundi ya nyota ya kusini.