12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!Jinsi ulivyokatwa kabisa,Ewe uliyewaangusha mataifa!
13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni,Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu;Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,Katika pande za mwisho za kaskazini.
14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu,Nitafanana na yeye Aliye juu.
15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu;Mpaka pande za mwisho za shimo.
16 Wao wakuonao watakukazia macho,Watakuangalia sana, wakisema,Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia,Huyu ndiye aliyetikisa falme;
17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake;Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?
18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima,Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;