33 Selofehadi, mwana wa Heferi hakupata watoto wa kiume bali wa kike tu, nao ni Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirza.
34 Hizo ndizo koo za Manase, jumla wanaume 52,700.
35 Kabila la Efraimu lilikuwa na jamaa za Shuthela, Bekeri na Tahani.
36 Ukoo wa Erani ulikuwa na jamaa ya Shuthela.
37 Hizo ndizo koo za Efraimu, jumla wanaume 32,500. Zote hizo zilitokana na Yosefu.
38 Kabila la Benyamini lilikuwa na jamaa za Bela, Ashbeli, Ahiramu,
39 Shufamu na Hufamu.