10 Viongozi wa Yuda wamekuwawenye kubadili mipaka ya ardhi.Mimi nitawamwagia hasira yangu kama maji.
11 Efraimu ameteswa,haki zake zimetwaliwa;kwani alipania kufuata upuuzi.
12 Hivyo mimi Mungu niko kama nondo kwa Efraimu,kama donda baya kwa watu wa Yuda.
13 Watu wa Efraimu walipogundua ugonjwa wao,naam, watu wa Yuda walipogundua donda lao,watu wa Efraimu walikwenda Ashurukuomba msaada kwa mfalme mkuu;lakini yeye hakuweza kuwatibu,hakuweza kuponya donda lenu.
14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu,kama mwanasimba kwa watu wa Yuda.Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka,nitawachukua na hakuna atakayewaokoa.
15 Nitarudi mahali pangu na kujitenga naompaka wakiri kosa lao na kunirudia.Taabu zao zitawafundisha wanitafute, wakisema: