28 Walichukua kondoo na mbuzi, ng'ombe, punda na chochote kilichokuwa mjini au shambani.
29 Waliteka nyara mali yote, watoto na wanawake wote na chochote kilichokuwa majumbani.
30 Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi, “Nyinyi mmeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakazi wa nchi hii ya Wakanaani na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”
31 Hao ndugu wawili wakajibu, “Ana haki gani ya kumtendea dada yetu kama malaya?”