3 Vilevile chukua ndege wa angani dume na jike, saba saba, ili kuzihifadhi hai aina zao duniani.
4 Baada ya siku saba, nitanyesha mvua nchini siku arubaini mchana na usiku, na kila kiumbe hai nilichokiumba duniani nitakiangamiza.”
5 Noa akafanya yote kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru.
6 Noa alikuwa na umri wa miaka 600 wakati gharika ilipotokea nchini.
7 Noa, mkewe, wanawe na wake zao wakaingia ndani ya safina ili kuiepa gharika.
8 Wanyama walio safi, wanyama walio najisi, ndege na viumbe vyote vitambaavyo,
9 wawiliwawili, dume na jike, wakaingia ndani ya safina pamoja na Noa kama Mungu alivyomwamuru.