2 Wanyama wote, ndege wote wa angani, viumbe wote watambaao juu ya nchi na samaki wote wa baharini watakuwa na hofu na kuwaogopa nyinyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu.
3 Wanyama wote hai watakuwa chakula chenu kama vile nilivyowapa mimea kuwa chakula chenu.
4 Lakini msile nyama yenye damu, kwani uhai uko katika damu.
5 Damu ya uhai wenu nitaidai; nitaidai kutoka kwa kila mnyama na binadamu. Atakayemuua binadamu mwenzake, nitamdai uhai wake.
6 Amwagaye damu ya binadamu,damu yake itamwagwa na binadamu;maana binadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu.
7 Nanyi zaeni, mkaongezeke;zaeni kwa wingi, mkaongezeke nchini.”
8 Kisha Mungu akamwambia Noa na wanawe,