45 ambayo baba zetu, kwa kupokezana, wakaiingiza pamoja na Yoshua katika milki ya Mataifa wale, ambao Mungu aliwafukuza mbele ya baba zetu, mpaka siku za Daudi;
46 aliyepata fadhili mbele za Mungu, naye aliomba ampatie Mungu wa Yakobo maskani.
47 Lakini Sulemani alimjengea nyumba.
48 Ila Yeye aliye juu hakai katika nyumba zilizofanywa kwa mikono, kama vile asemavyo nabii,
49 Mbingu ni kiti changu cha enzi,Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu;Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana,
50 Au ni mahali gani nitakapostarehe?Si mkono wangu uliofanya haya yote?
51 Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.